CHELSEA NAO KUONGEZA DAU KWA ROONEY - MAGAZETI YA ULAYA LEO

Chelsea wako tayari kuongeza dau mpaka kufikia £30m kwa straika Rooney, gazeti la the Daily Mail limeandika. Ofa ya mwanzo iliyokua £25m ilikataliwa ila kwa sasa the Blues hawaoni taabu kuongeza mpaka kufikia £30m na kumlipa Rooney mshahara wa £240,000 kwa-wiki.
Ilhali, the Daily Star lenyewe limeandika kwamba Rooney meonekana akicheza mchezo wa golf katika klabu ya gofu iliyopo karibu kabisa na kiwanja cha mazoezi cha Chelsea(Cobham) - kiwanja ambacho wachezaji wengi wa Chelsea hupenda kucheza pia. Inamaanisha nini? wewe mwenyewe pigia mstari.

Maoni ya FullSoka: Nionavyo, Rooney kucheza golf katika kiwanja kilicho karibu na viwanja vya mazoezi vya Chelsea, jambo hilo halina uhusiano wowote na uwezekano wa jamaa huyo kuhamia Chelsea - nachojua ni kwamba Jose Mourinho anamtaka sana na Rooney nae anataka sana kuondoka, ila mzigo upo kwa mchezaji mwenyewe kuiandikia United barua rasmi ya kutaka kuondoka - ingawa inajulikana United imedaiwa hata kwa hali hiyo watagoma kumuuza ila nionavyo mimi ikifikia hatua hiyo basi itabidi wanyanyue mikono na kumuuuza.

Vyanzo - (Daily Mail) & (Daily Star).

Subscribe

Flickr