‘Ongezeko linachangia wanafunzi kuacha shule’

Dar es Salaam. Shirika lisilo la Kiserikali la Children’s Dignity Forum (CDF), limebainisha kuwa ongezeko la watu katika miji mikubwa nchi linachangia wanafunzi wengi kushindwa kumaliza elimu ya msingi na sekondari.
Mkurugenzi Mtendaji wa CDF, Koshuma Mtengeti, alibainisha hayo jana katika uzindizi wa ripoti ya watoto na miji nchini.
Alisema, kutokana na wingi wa watu wanaoishi mijini na mrundikano wa magari,, watoto wengi wamekuwa wakishindwa kumaliza elimu kwa sababu hakuna magari ya kuwapeleka shule.
“Katika majiji mengi kumekuwa na wimbi kubwa la watoto wanaoshindwa kumaliza elimu kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamopja na kukosekana kwa magari ya kuwapeleka shule,” alisema Mtengeti.
Alisema, kutokana na wingi huo wa familia nyingi pia zimekuwa na maishi magumu.
“Katika hili utawakuta vijana wengi wameacha shule na kuanza kufanya kazi za ndani, ukahaba na hatimaye watoto wenye kati ya umri wa miaka 10 hadi 18 ndiyo wanaopata maambukizi ya virusi vya ukimwi,” alisema.
Alibainisha kuwa kutokana na hali hiyo wako katika mchakato wa kupanga pamoja na manispaa zote za majiji hayo ili kutengeniza mpango wa pamoja wa kutatua changamoto zinazowakumba watoto hao.
SOURCE,MWANANCHI

Subscribe

Flickr