Mapendekezo ya (CCM) kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya

Mapendekezo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wanachama na viongozi wake.
UTANGULIZI
1.1 Mnamo tarehe 03/06/2013 Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilitangaza rasimu ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1.2 Rasimu hii ya Katiba itajadiliwa katika mfumo wa aina mbili wa mabaraza:
Mabaraza ya Katiba ya Wilaya, ambayo yameshaundwa na yatatoa maoni yake kupitia mikutano itakayoitishwa na Tume ya Marekebisho ya Katiba. Mabaraza haya yanasimamiwa na Tume yenyewe.
Mabaraza ya Asasi, Taasisi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana kama vile vyama vya siasa na jumuiya za kidini na kadhalika. Mabaraza haya yanasimamiwa na Asasi au Taasisi husika.
1.3 Chama Cha Mapinduzi kimeshajiunda kama Baraza la Katiba la kitaasisi na kutambuliwa rasmi na Tume kwa barua Kumb.na. AB 76/386/57 ya tarehe 24/052013
1.4 Kwa kuzingatia kwamba Chama Cha Mapinduzi ni Taasisi muhimu na yenye masilahi makubwa katika upatikanaji wa Katiba Mpya, Kamati Kuu ya Halmashauri ya Taifa iliyokutana mjini Dodoma Tarehe, 10/6/2013, pamoja na mambo mengine ilielekeza kwamba uandaliwe utaratibu utakaohusisha utoaji wa maoni utakaotumiwa na wanaCCM kutoa maoni yao.
1.5 Madhumuni ya ufafanuzi huu ni kujenga uelewa wa pamoja wa maudhui ya Rasimu ya Kwanza na hivyo kuwawezesha wanaCCM kushiriki kutoa maoni yao kikamilifu kutoka ngazi ya matawi hadi taifa.
UTARATIBU WA KUTOA MAONI
2.1 Kwa upande wa matawi maoni yatatolewa kupitia mikutano
Kwa wilaya, mikoa na taifa. Maoni yatatolewa kupita halmashauri kuu zao.

Subscribe

Flickr